Posts

Showing posts from April, 2017

MAGAZETI YA LEO MAY 1 ,2017

Image

Xi jinping amuunga mkono Trump

Image
Rais wa Marekani, Donald Trump amemsifu rais wa China, Xi jinping kwa kuiunga mkono Marekani na jitihada zake za kupambana na mpango wa Nuklia wa Korea kaskazini. Trump amesema kupata ushirikiano huo wa kupambana na Pyongyang ilikuwa muhimu kuliko kuishinikiza Beijing kuhusu masuala ya biashara. Rais Donald Trump amesema aliamini kuwa Rais Xi alikuwa akiishinikiza Korea kaskazini, ikitaka, mazungumzo yafanyike kuhusu silaha za Nuklia za Kim Jong Un ''Rais wa China, Rais Xi, ninaamini amekuwa akimshinikiza pia.lakini mpaka sasa, pengine hakuna kilichotokea na pengine kimetokea. Hili lilikua kombora dogo, halikuwa kombora kubwa, halikuwa jaribio la Nuklia, ambalo alitegemewa kulitekeleza siku tatu zilizopita, tutaona nini kitakachoendelea'' Trump ametahadharisha kuwa mgogoro wowote wa kijeshi na Korea kaskazini unaweza kugharimu maisha ya mamilioni ya watu. Aliyasema hayo kwenye mahojiano na chombo cha habari cha CBS cha Marekani ambapo alizungumzia hali ya...

YANGA YAVULIWA UBINGWA NA MBAO FC

Image
Klabu ya soka ya Mbao fc ya jijini Mwanza nchini Tanzania Jana imefanikiwa kuwafunga Mabingwa wa soka Tanzania bara na Kombe la Shirikisho Tanzania klabu ya Yanga Bao 1-0 kwa bao la kujifunga kupitia kwa Vincent Andrew 'Dante' na kutinga hatua Fainali . Hivyo kwa matokeo hayo sasa Mbao fc mwishoni mwa juma hili watakutana na Simba Sc katika hatua ya fainali. Simba sc Klabu wao walifanikiwa kutinga fainali ya michuano hiyo kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Azam fc , Mshindi wa Kombe hili ndie atakayeiwakilisha Tanzania Bara katika Mashindano ya Kombe la Shirikisho kwa Msimu ujao.

VIDEO ; RAIS MAGUFULI ASHIRIKI IBADA MOSHI (KKKT)

Image
ANGALIA VIDEO HII HAPA CHINI

JPM ;Atoa milioni moja kusaidia wanakwaya kurekodi

Image

MARK ZUCKEERBERG ; aitembelea kwa ghafla familia moja Ohio

Image
Familia moja nchini Marekani imeeleza ilivyohisi wakati ilipata taarifa kwamba mwanzilishi wa mtandao wa kijamii wa Facebook Mark Zuckerberg angewatembelea kwa chakula cha jioni. Familia hiyo ya Moore , eneo la Newton Falls, inasema walijua utambulisho wa mgeni wao dakika 20 kabla ya kuwasili ijumaa. Bwana Zuckerberg anazuru majimbo yote 50 ya Marekani na amewataka wafanyikazi wake kutafuta wanachama wa Democrat waliompigia kura rais Donald Trump. Anakisiwa kuwa na mpango wa kuwania urais wa Marekani. Familia hiyo inasema bwana Zuckerberg alikuwa mtu mtulivu sana.

video; mashuhuda wa tetemeko wasimulia ilivyokuwa

Image
Habari nyingine kubwa kutokea Bukoba usiku wa kuamkia April 30, 2017 ni kuhusu tetemeko la ardhi video hii hapa chini mashuhuda wanasimulia kilichotokea mwanzo mwisho angalia video hii hapa chini BONYEZA HAPA KUANGALIA MAJINA YA WALIOTUMBULIWA

WASOMI WAZUA MJADALA ,KUHUSU VYETI FEKI

Image
Wasomi wamepinga kufanyika kwa ubaguzi wa wenye vyeti feki kwa kuwaacha baadhi ya mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya katika uhakiki huo. Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya Rais John Magufuli kuagiza wafanyakazi 9,932 waliobainika kuwa na vyeti feki, waondolewe kazini. Uamuzi huo wa Serikali umesaidia kunusuru kutumika kwa fedha nyingi kuwalipa watu wasiokuwa na sifa. Kama watumishi hao wote wanalipwa kiwango cha kima cha chini cha mshahara cha Sh300,000 jumla ya Sh35.7 bilioni zimekuwa zikitumika kila mwaka kuwalipa. Wakati akikabidhi orodha hiyo juzi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki amesema kazi hiyo haikuwagusa mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kwa kuwa wao wanatakiwa kujua kusoma na kuandika. Kauli hiyo imeibua mjadala mzito kwa kile kilichodaiwa inalenga kutetea uovu na kuhalalisha mambo yasiyofaa bila kuangalia wakati uliopo. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Bashiru Ally am...

Bayern Munich bingwa tena Ujerumani.

Image
Ushindi wa mabao 6 kwa 0 waliopata dhidi ya Wolfsburg uliwafanya Bayern Munich kuchukua tena ubingwa wa ligi ya Ujerumani almaarufu kama Bundesliga. Hii ilikuwa mara ya tano mfululizo kwa timu hiyo kutwaa kombe hilo kwani kuanzia mwaka 2013,2014,2015,2016 na mwaka huu Bayern wamebeba kombe hilo. Hili ni kombe la kwanza kwa kocha Carlo Ancelotti toka ajiunge na Bayern msimu huu lakini linaweza kuwa la mwisho kwa kapteni wa timu hiyo Philip Lahm ambaye ameshashinda mataji 9 na timu hiyo. Lahm alishatangaza nia yake ya kutundika daluga mara baada ya msimu huu kuisha na pia kiungo Xabi Alonso naye anaweza kufuata nyayo za Lahm mwishoni mwa msimu huu. Wakati Bayern wakichukua ubingwa, huko nchini Hispania bado Real Madrid na Barcelona wanakimbizana kama kawaida kuwania ubingwa wa La Liga msimu huu. Real Madrid waliibuka kidedea kwa kuibamiza Valencia mabao mawili kwa moja lakini baadae Luis Suarez alifunga mawili na Messi moja na kuifanya Barcelona kuibuka kidedea k...

Tupofiti kuivaa Mbao FC.(Mwambusi)

Image
Kocha msaidizi wa Yanga SC, Juma Mwambusi amesema wapo tayari kuwavaa Mbao FC na wamewaomba mashabiki wa klabu hiyo waliopo Mwanza na mikoa ya jirani wafike kuwapa sapoti na kushuhudia mpira safi toka kwa vijana wao. Mwalimu huyo amesema hawezi kuidharau Mbao FC kwani ni timu nzuri na yenye ushindani mkubwa hivyo wanahitaji kucheza kwa tahadhari na umakini mkubwa ili kuibuka na ushindi wa pointi zote tatu. "Tumejiandaa vyema na tunamshukuru Mungu tumemaliza mazoezi yetu salama na tupo tayari sasa kuwavaa Mbao Fc, kikubwa mashabiki wetu wa Mwanza na mikoa ya karibu wafike kwa wingi waje kuona mpira safi kabisa toka kwa vijana wao na tunaamini ata Mbao nao wataonyesha mpira mzuri na waupinzani mkubwa"-Juma Mwamusi Mwalimu Yanga SC. Aidha, katika mchezo huu wa nusu fainali ya Kombe la FA utakaochezwa leo saa kumi jioni katika viwanja vya CCM Karumba, Jijini Mwanza mshindi wake atakutana kwenye fainali na Simba SC iliyoshinda goli 1:0 dhidi ya Azam FC jana.

Zitto Kabwe ahoji viwango vya ubora wa ndege( Dreamliner)

Image
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe amehoji viwango vya ndege inayonunuliwa na Serikali aina ya Dreamliner akisema ndege hizo zilikataliwa na mashirika mengine ya dunia kutokana na ubora wake. Hiyo ni moja kati ya ndege ambazo Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli imepanga kuzinunua katika mkakati wake wa kulifufua Shirika la Ndege Tanzania (ATCL). Tayari imeshanunua mbili aina ya Bombardier. Zitto alisema hayo katika mchango wake wa maandishi kuhusu hotuba ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano juzi usiku. Mjadala huo wa siku tatu utaendelea Jumanne ijayo ambapo Waziri Makame Mbarawa atajibu hoja za wabunge. “Ndege hizi zinaitwa ‘Terrible Teens Dreamliners’ ambazo zilikuwa 12 na zilikosa soko kwa sababu ni nzito na hazina viwango,” alisema. Alisema pia Ethiopia imenunua ndege hizo lakini kwa punguzo kubwa la bei kwa sababu hazikuwa na soko. “Wajibu wangu kama mbunge ni kuisimamia Serikali na kuhakikisha fedha za ...

Magazeti ya leo jumapili April 30 ,2017

Image